Adverts

Feb 21, 2013

JESHI LA ULINZI LA ZIMBABWE KUTOA ULINZI KWENYE SHOW ZA MASTAA WATATU NCHINI HUMO


 Mwanamziki Alick Macheso akiwa na kundi lake katika moja ya ziara zake nchini Uingereza mwaka jana mwezi November (wa katikati shati lenye wekundu na jaketi jeusi)
sehemu ya Minjonjo ya Alick Macheso katika upigaji wake gitaa ambapo hutumia miguu yake kukung'uta kitu mpini!!!!! bongo nani anaweza?.
na Danny Tweve wa Indaba Blog kwa msaada wa website ya Alick Macheso na Zimbabwean Breaking News

Serikali ya Zimbabwe imesema itatoa ulinzi kupitia jeshi lake la ulinzi ZNA wakati wa onyesho la wanamziki watatu maarufu nchini humo ALICK MACHESO,SULUMAN CHIMBETU na JAH PRAYZAH .
Aidha jeshi hilo limeahidi kuendea kutoa ulinzi kwa shughuli za wanamziki hao nchini mwao hatua ambayo itafanya wanamziki hao kuwa wa kwanza kulindwa na jeshi la nchi katika shughuli zao za kimziki .
Kwa watu wengine wanaweza kudhani kuwa mtu maarufu nchini Zimbabwe kwa muziki wake ni Oliver Mtukudzi, lakini hali siyo hiyo kwani Oliver Mtukudzi amebaki kuheshimika kama mzee aliyeiongoza sanaa katika utunzi wa nyimbo za busara
Alick Macheso ndiye chaguo la wazimbabwe wengi katika nyimbo zake alizotoa katika album zipatazo 18 katika vipindi tofauti huko nyuma, mtindo wao wa upigaji vyombo kwa kasi (miziki ya zamani ya kwenye santuri enzi hizo ikitoka Kenya  na Zimbabwe kama mangerengere ndiyo staili inayouza mziki nchini Zimbabwe .
Kwa mujibu wa Zimbabwean Breacking News, wanamziki hao watatu watafanya show hiyo kwenye uzinduzi wa mchezo wa ngao ya hisani kwaajili ya kuadhimisha mwaka wa Jeshi la Zimbabwe ZNA , mchezo unaotarajiwa kufanyika katika uwanja wa Rufaro  kati ya Timu ya Jeshi hilo Black Rhinos  na CAPS  united.
Akizungumza kwa niaba ya Kamanda mkuu wa ZNA Luteni Generally Philip Valerio Sibanda , Brigedia Generali Howard Matombo alisema wanamziki hao wamekuwa waaminifu  kwa jeshi la Zimbabwe kutokana na ushiriki wao wakati wote tangu kuanzishwa kwa michezo ya ngao ya hisani ya jeshi hilo
Alick Macheso ambaye hata mmiliki wa mtandao wa Indaba blog ni shabiki wake kutokana nakujaza miziki yake nyumbani anawika hivi sasa na albam yake ya Kwatakabva Mitunhu”aliyotoa Disemba 05, 2012 huku akiingiza mwanamziki mpya kwenye bendi yake Kochekera.
Hata hivyo katika ukurasa wa website yake Macheso anawaomba mashabiki wake waendelee kumwombea mwanamziki wake mpiga gitaa Luckie Yahwe Mayor Mumiriki ambaye alipata stroke na sasa anapata matibabu na mazoezi

sehemu ya maneno yake ALICK MACHESO KWENYE MTANDAO WAKE  jana!

Please continue to pray for my sub-rhythm player, Luckie 'Yahwe Mayor' Mumiriki, who is still struggling to for muscle healing, following the stroke he suffered. Luckie has been a core member of my band for years, it's painful not to see him on stage doing what he does best. With your prayers and support, we hope to have Luckie back doing what he does best.