Adverts

May 25, 2013

MEELA ASIKIKITISHWA NA HALI YA WANAHABARI MBEYA, ATIA MKONO KUANZISHA SACCOS


MKUU wa wilaya ya Rungwe Bw. Chripin Meela amesema, changamoto zinazokabili sekta ya habari na  vyombo vya habari  kwa ujumla ni matokeo ya umuhimu wa taaluma hiyo katika ukuaji wa demokrasia nchini
Akizungumza kwenye mkutano wa uchaguzi wa klabu ya wandishi wa habari mkoa  Mbeya unaoendelea ukumbi wa Royal Tughimbe, Mkuu wa wilaya ya Rungwe Chrispin Meela amesema, wananchi wana matumaini makubwa na vyombo vya habari na pale kipapota doa la utendaji ni muhimu kujirekebisha kabla ya kutengeza picha mbaya mbele ya jamii wanayoihudumia
Amesema hali iliyojitokeza hivi karibuni kwenye klabu hiyo inahitaji kuweka misingi imara ya kiutendaji  na kwamba jitihada za kufanya uchaguzi  wakati huu ni hatua muhimu za kuimarisha mfumo wa kujiwajibisha kama taasisi ya taaluma.
Amesema ikiwa viongozi wa dini na vyombo vya habari vitajihusisha na ubadhirifu na wizi ni dalili kuwa hakutakuwa na mwingine wa kukemea jamii itakayokuwa huru na yenye kukemea vita dhidi ya rushwa
Bwana Meela amesema inashangaza kuona hata vyombo vya habari vinaingia kwenye ufisadi na akaohoji  ninani atakayehoji ufisadi serikali na kwingineko kama nanyi mnaingia kwenye mitego hiyo hiyo?
Katika hatua nyingine amependekeza  Vyombo vya habari kujenga utamaduni wa kujihusisha na ufuatiliaji wa maendeleo vijijini na kwa kufanya hivyo kutawezesha wananchi kuwasilisha changamoto zinazowakabili kwa watunga sera.
Amesema katika kufikia hilo  ni vyema pia Viongozi wa serikali ngazi za chini kuondoa uoga  katika kufanya kazi na vyombo vya habrari na kwa kufanya hivyo kutasadia kusukuma mbele jitihada za maendeleo
Katika hatua nyingine Bwana Meela amechangia kiasi cha shilingi 400,000 kwaajili ya uanzishaji wa chama cha kuweka na kukopa cha wanahabari  SACCOS  ili kuwezesha kuwapa fulsa wana habari  kujisimamia kiuchumi  na kupunguza changamoto za kimaisha zinazowakabili
Katika kufanikisha hilo wanachama wa Mbeya Press club walijitokeza kuchangishana wenyewe ambapo wamefanikiwa kukusanya mtaji wa papo kwa papo kiasi cha shilingi 1,400,000/=
Aidha ameshauri klabu ya wandishi wa habari kuwa na ofisi yake na hvyo kwa kuomba kiwanja kwenye mamlaka za majiji itasaidia kuwapa nguvu katika kusimamia haki zao wakiwa na uhuru wa kuwekeza kwenye majengo yao.