Adverts

Jun 30, 2013

KIMONDO SUPER SPORT CLUB YAINGIA DARAJA LA KWANZA KWA KUIGAGADUA POLISI JAMII BAO 3-1


PICHA ZOTE NA CAPTIONS KWA HISANI YA MWANAFASIHI(MAHIRI WA SIMULIZI BLOG).


WACHEZAJI WA TIMU YA KIMONDO WAKIPEANA MIKONO NA WACHEZAJI WA TIMU YA POLISI JAMII, KABLA YA KUANZA KWA MECHI YA LIGI YA MABINGWA WA MIKOA KATIKA UWANJA WA SOKOINE LEO JIONI


TIMU YA POLISI JAMII YA BUNDA-MARA


TIMU YA KIMONDO FC YA MBOZI-MBEYA


GOLIKIPA WA TIMU YA POLISI JAMII  EMANUEL DAUD AKISHANGAA GOLI LILILOFUNGWA NA MCHEZAJI WA TIMU YA KIMONDO CHARLES HIZA DK YA 12


GOLI LILIPITILIZA NA KUPENYA KWENYE NYAVU NA KUSABABISHA REFARII NA VIONGOZI WA CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU MKOA WA MBEYA KUREKEBISHA NYAVU HIZO KWA DAKIKA KADHAA KABLA YA MPIRA HAUJAWEKWA KATI












Add caption








GOLI LA TATU KWA UPANDE WA KIMONDO BAADA YA MPIRA WA PENALT GOLI LILIFUNGWA NA MCHEZAJI LUKA MPOSHI DK 59


WACHEZAJI WA TIMU YA KIMONDO WAKISHANGILIA GOLI








KIPUTE KINAENDELEA UWANJANI




PATASHIKA KATIKA GOLI LA POLISI JAMII




NDEREMO NA HOI HOI ZILITAWALA BAADA YA KIPYENGA CHA MWAMUZI KUPILIZWA HUKU KIMONDO FC IKIWA MBELA KWA MABAO 3-1


POLISI WALILAZIMIKA KUMTOA NJE YA UWANJA REFARII KUTOKANA NA KUZONGWA NA WACHEZAJI WA TIMU YA POLISI JAMII MARA BAADA YA KUMALIZIKA KWA MCHEZO




HOI HOI ZA FURAHA ZINAENDELEA


MASHABIKI WAKIWA WAMEMNYANYUA JUU MWENYEKITI WA TIMU HIYO ELICK AMBAKISYE BAADA YA TIMU HIYO KUJIHAKIKISHIA KUCHEZA LIGI KUU TANZANIA BARA








SHANGWE NA HOI HOI ZINAENDELEA KATIKA DIMBA LA KUMBUKUMBU YA SOKOINE MKOANI MBEYA






KOCHA WA TIMU YA POLIS JAMII MADENGE OMAR AKILALAMIKIA UTARATIBU WA UENDESHAJI WA LIGI HIYO


PONGEZI ZINAENDELEA


'TUMESHINDA TUNAMSHUKURU MUNGU TUMEPITIA VIGINNGI NA VIKWAZO VINGI'' AKIONEKANA ANASEMA MWENYEKITI WA TIMU HIYO ELICK MINGA






SHABIKI WA TIMU YA KIMONDO MBEGU MOJA AKIWAZAWADIA WACHEZAJI WA TIMU HIYO SH. 200,000 BAADA YA USHINDI






Na DannyTweve

Timu ya Kimondo super sports club ya Mbozi mkoani Mbeya imeungana na ... kuingia daraja la kwanza Tanzania bara baada ya kumaliza mchezo wake jana kwa kuifunga timu ya Polisi jamii ya Bunda mkoani mara mabao 3 -1.

Katika mchezo mzuri na wakasi uliofanyika uwanja wa sokoine jijini Mbeya ulishuhudia Polisi Jamii wakicheza kufa na kupona licha ya maelezo ya kocha wao kuwa walishtukizwa mchezo huo kwani TFFA awali walitangaza kuwa ungechezwa siku ya jumapili.

Bao la kwanza la Kimondo liliwekwa wavuni mnamo dakika ya 12 kupitia kwa Charles Hiza baada ya kupokea pasi kutoka kwa Geofrey Mlau na kumchungulia mlindamlango wa Polisi Jamii Emmanuel Daud na hatimaye kumchambua na kuhesabu bao la kwanza

Mashambulizi ya hapa na pale yaliendelea kwa timu zote ambapo mnamo dakika ya  17 Cosmas Mwazembe wa Kimondo SSC aliunganisha wavuni kwa kichwa krosi ya Charles Hiza na kuifanya Kimondo kuongeza hamasa kwa mabao 2 ya haraka haraka waliyoyapata.

Hata hivyo sherehe hiyo ilidumu kwa dakika 30 tu kwani Polisi jamii kupitia kwa Joseph Onyango waliweza kuihada ngome ya Kimondo na kuachia shuti kali lililodakwa na kutemwa kwenye nyavu na kipa wa Kimondo Daud Pius ha hivyo kuwafanya Polisi Jamii kutoka kipindi cha kwanza wakiwa na matumaini ya kurejesha bao la jingine katika kipindi cha pili.

Bao la tatu kwa Kimondo lilifungwa mnamo dakika ya 59  kwa njia ya penati kupitia kwa Lucas Baraka baada ya mshambuliaji Geofrey Mlau kuangushwa eneo la hatari katika purukushani za kumdhibiti akiwa njiani kwenda langoni mwao.

Mnamo dakika ya 57 mwalimu wa Polisi jamii Bunda  Madenge Omary alitolewa eneo la benchi la ufundi baada ya kumtukana  mwamuzi wa mchezo huo Daudi Ahadi kutoka jijini Dar es Salaam  na akizungumza baada ya mchezo huo, alisema wachezaji wake wamechezeshwa wakiwa wamechoka kutokana na kuwasili asubuhi jijini Mbeya na kulazimishwa kucheza wakati TFF ilikuwa imetangaza mchezo huo kuchezwa siku ya jumapili na si jumamosi.

Akizungumzia kupanda daraja kwa timu yao Mkurugenzi wa Timu ya Kimondo Erick  Minga ndoto za wilaya ya Mbozi kuwa mkoa zinakwenda sambamba na ukuzaji wa soka wilayani humo ambapo watahakikisha timu yao inapanda daraja na kuingia ligi kuu msimu ujao na kuwataka wananchi wa mkoa wa mbeya kwa ujumla kushiriki katika kuchangia mafanikio ya timu zao.

Alisema tayari sasa mkoa utakuwa na michezo mfululizo katika uwanja wake wa sokoine kwa kuwa kuna timu mbili za ligi kuu, pia Kimondo itavuta michezo ya daraja la kwanza hatua ambayo wananchi watafadi uhondo wa soka mkoani mwao kwa mwaka  mzima.