Adverts

Jun 27, 2013

MBOZI YAENDELEA KUKABILIWA NA CHANGAMOTO ZA MAJI SAFI NA SALAMA


Na Angela Kivavala- Mbozi   

Asilimia 44   wakazi wa wilaya ya Mbozi ndiyo wanaopata huduma ya maaji safi na salama imefahamika

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari mkugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya Mbozi Levison Chillewa amesema kwa sasa wilaya inategemea aina tatu za vyanzo vya maji vikiwemo  visima, mitiririko na maji ya chemichemi zilizo boreshwa.

Akifafanua  Chillewa amesema  kuna  jumla ya  visima virefu na vifupi 105 chemichemi za asili 40 mitiririko 5 na matanki 6 yanayotumika kuvuna  maji ya mvua.

Chillewa amesema kupitia programu ya maji na usafi wa mazingira vijijini (RWSSR),wilaya inatekeleza  miradi ya ujenzi  wa  miundombinu  ya maji katika wilaya ya mbozi ambapo hadi sasa visma vitano vinajengwa ikiwa ni vyanzo vya usambazaji wa maji katika vijiji vitano vya wilaya ya mbozi

Aidha Kupitia mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF, halmashauri ya wilaya ya Mbozi   imewezesha baadhi ya shule za sekondari na  hususani miradi ya ujenzi wa hosteli pamoja na baadhi ya huduma kama zahanati na nyumba za walimu kuwa na  mfumo wa uvunaji wa maji ya mvua  kwa kuwekewa  tanki za plastiki (SIMTANK) zenye ujazo wa kati ya lita 5000 hadi lita 10,000.

Kuhusiana na uhifadhi wa mazingira, Mkurugenzi huyo amesema wilaya ya mbozi vyanzo vya 23 tayari vimepimwa na vipo kwenye hatua za kuwekewa alama za kudumu.

 aidha halmashauri ya wilaya imeanzisha mfumo wa  kuifadhi takwimu  za vyanzo vya maji ambapo hadi mwezi mei jumla ya vyanzo vya maji 471 vilikuwa vimetambuliwa pia vyanzo vya maji vimepewa kipaumbele na kamati za maendeleo za vijiji na kata.

Pamoja na mafanikio wilaya imekuwa ikikumbanana changamoto mbalimbali ikiwemo uharibifu wa vyanzo vya maji unaotokana na kulima kujenga kuchoma moto na kuchunga mifugo kwenye vyanzo vya maji na gharama kubwa za uchimbaji na ujenziwa miundombinu ya maji.

Wilaya imeweza kuwekamikkati ya kuzikabili changamoto hizo ikiwa nipamoja na  kuelimisha jamii kuusu umuhimu wa tuunzaji wa vyanzo vya maji kulinda na kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchiikiwa ni pamoja na upandaji wa miti  katika vyanzo vya maji, vijiji vyote vyawilaya vimepewa jukumula kudhibiti uharibifu katika vyanzo vya maji

Kwa mwaka 2013/ 2014 halmashauri imetengewa TSH 1,425,470,049 kwaajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya maji wilaya ya mbozi

Mwisho