Adverts

Nov 12, 2013

VIWANJA SABA VYA LIGI KUU NA LIGI DARAJA LA KWANZA VYAFUNGIWA


KATIBU WA MUDA WA TFF  BONIFACE WAMBURA 

Tanzania Football Federation
Affiliated to FIFA, CAF and CECAFA
Karume Memorial Stadium, Uhuru/Shaurimoyo RoadP.O. Box 1574, Dar es Salaam, Tanzania
.
 Telefax: + 255-22-2861815E-mail:tanfootball@tff.or.tz
 Website:www.tff.or.tz 

 Release No. 194TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARINovemba 12, 2013

BODI YA LIGI YAFUNGIA VIWANJA SABA
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board) imefungia viwanja saba vilivyokuwavikitumiwa na timu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza(FDL) hadi vitakapofanyiwa marekebisho ili kukidhi mahitaji ya mechi zampira wa miguu.Uamuzi huo umefikiwa na TPL Board katika kikao chake cha kwanzakilichofanyika juzi (Novemba 10 mwaka huu) jijini Dar es Salaam ambapopamoja na mambo mengine kilipitia ripoti za mechi za VPL na FDL katikamzunguko wa kwanza.

Viwanja vilivyofungiwa na marekebisho yanayotakiwa kufanyika kwanza iliviruhusiwe kutumika tena ni Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba (majukwaa yakeyamechakaa, hivyo kuhatarisha usalama wa watazamaji), na Uwanja wa CCMMkwakwani jijini Tanga (vyumba vya wachezaji kubadilishia nguo (dressingrooms) havina hadhi).Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya (sehemu ya kuchezea- pitchni mbovu), Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha(pitch ni mbovu), Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi (vyumba vya kubadilishiakutumika kwa ajili ya shule ya awali), Uwanja wa Majimaji mjini Songea(pitch ni mbovu) na Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro (pitch ni mbovu).

Klabu ambazo timu zake zinatumia viwanja hivyo zimeshaarifiwa rasmi juu yauamuzi huo ambapo ama vinatakiwa kuwasiliana na wamiliki wa viwanja hivyoili wafanye marekebisho au kutafuta viwanja vingine vya kuchezea mechi zao.Kwa upande wa ripoti za mechi za VPL; Mbeya City imepigwa faini ya sh.500,000 na kupewa onyo kali kwa timu yake ya U20 kutocheza mechi yautangulizi walipocheza na Yanga. Pia wanatakiwa kulipa gharama za uharibifubaada ya washabiki wao kuvunja kioo cha basi la Yanga baada ya gharamahizo kuthibitishwa na Bodi ya Ligi.

Pia Mbeya City imepigwa faini ya sh. 500,000 kwa washabiki wakekushambulia basi la wachezaji wa Tanzania Prisons baada ya mechi dhidi yao,na kulipa gharama za uharibifu baada ya kuthibitisha na Bodi ya Ligi.Coastal Union imepigwa faini ya sh. 500,000 kutokana na vurugu za washabikiwake ilipocheza na Azam kwenye Uwanja wa Mkwakwani ambapo mwamuzimsaidizi Hassan Zani alishambuliwa kwa mawe na kujeruhiwa mkononi nakichwa, tukio lililosababisha mchezo kusimama kwa dakika tatu.Beki wa Coastal Union, Hamad Khamis wa Coastal Union amepigwa faini ya sh.500,000 kwa kumpiga kichwa kwa makusudi Kipre Tchetche wa Azam.

Kitendo hicho kilisababisha refa amtoe nje kwa kadi nyekundu, hivyo atakosa mechitatu zinazofuata za timu yake.Mchezaji Cosmas Lewis wa Ruvu Shooting alifanya kitendo cha utovu wanidhamu kwa kupiga kelele wakati mgeni rasmi akisalimia timu na kukataakupeana mkono na kamishna kwenye mechi dhidi ya Rhino Rangers, hivyoamefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 500,000.Mtunza vifaa (Kit Man) wa JKT Ruvu, Selemani Oga aliondolewa kwenyebenchi la ufundi wakati wa mechi yao dhidi ya Mbeya City kwa kosa la kutoalugha chafu kwa refa, hivyo suala lake litapelekwa katika Kamati ya Maadili.Kocha Msaidizi wa Oljoro JKT, Fikiri Elias amepigwa faini ya sh. 500,000 nakufungiwa mechi tatu kwa kumshambulia kwa matusi refa wakati wa mechiyao dhidi ya Ashanti United.

Naye mtunza vifaa wa timu hiyo Elas Justinamepele kwa Kamati ya Maadili kwa kumshambulia refa kwa matusi ya nguoni.Simba wamepigwa faini ya sh. 500,000 kutokana na vurugu za washabiki wakewakati wa mechi dhidi ya Kagera Sugar.Katika FDL, mchezaji Ally Mtoni wa Villa Squad amepigwa faini y ash. 200,000na kufungiwa mechi tano. Kosa lake ni kujisaidia haja ndogo golini wakti wamechi dhidi ya Ndanda FC iliyochezwa mjini Mtwara.

Kamishna Paul Opiyo wa mechi ya FDL kati ya Villa Squad na Transit Campkwa kutokuwa makini. Katika ripoti yake ameeleza kuwa Transit Campilichelewa kufika uwanjani, lakini hakusema ilichelewa kwa muda gani.Kocha wa Polisi Dar es Salaam, Ngelo Nyanjabha na Meneja wa timu hiyoMrimi Masi wamepigwa faini ya sh. 200,000 na kufungiwa mechi tatu kilammoja kwa kuongoza kundi la washabiki kumvamia refa wa mechi yao dhidiya Villa Squad iliyochezwa Dar es Salaam.

Pia Bodi ya Ligi imeagiza Polisi waandikiwe barua ya onyo kwa vile wakatiwaamuzi wanapigwa walikuwepo lakini hawakutoa msaada kwa wakati.Kocha wa Friends Rangers, Kheri Mzozo amepigwa faini ya sh. 200,000 nakufungiwa mechi sita kwa kosa la kumtukana refa na kutishia kuhamamishawashabiki waingie uwanjani kufanya fujo kwenye mechi dhidi ya Villa Squad.Naye Kocha msaidizi wa timu ya Transit Camp, Haji Amiri amepigwa faini yash. 200,000 na kufungiwa mechi sita kwa kutoa lugha ya matusi kwa mwamuziwa akida wakati wa mechi dhidi ya Friends Rangers.Adhabu zote zimetolewa kwa mujibu wa kanuni.

Pia Bodi ya Ligi imeahirishakufanya uamuzi wa mechi kati ya Stand United na Kanembwa JKT iliyochezwaUwanja wa Kambarage ili kukusanya taarifa zaidi. Mechi hiyo haikumalizika.Bodi ya Ligi itakutana tena Jumapili (Novemba 17 mwaka huu).


FUTURE TAIFA STARS vs TAIFA STARS UWANJANI KARUME
Timu za Taifa za Future Taifa Stars na Taifa Stars zinacheza kesho (Novemba13 mwaka huu). Mechi hiyo ya kirafiki itafanyika Uwanja wa Kumbukumbu yaKarume jijini Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.Mechi hiyo ni maalumu kwa Benchi la Ufundi la Taifa Stars linaloongozwa naKim Poulsen kuangalia wachezaji kumi kutoka Future Taifa Starswatakaoongezwa katika Taifa Stars tayari kwa mechi ya kirafiki ya kimataifaitakayochezwa Novemba 19 mwaka huu jijini Arusha.Watazamaji 300 tu wataruhusiwa kushuhudia mechi hiyo kwa kiingilio cha sh.5,000.