Adverts

Mar 18, 2014

NDEGE WA AJABU BUKOBA WAZIDI KULETA MAAFA, SASA YABAINIKA KUSABABISHA MAGONJWA YA NGOZI

Sakata la ndege wa ajabu katika kisiwa cha Musira mkoani Kagera wanaotoa kinyesi kinachodaiwa kuwa na sumu na kusababisha kuku na mbuzi kuteketea sasa taarifa za kitaalum zimedai kuwa  7% ya  watoto na 3% watu wazima wameathiriwa na kinyesi kutokana na kushindwa kupumua vyema.

  Hayo ni  sehemu ya matokeo ya dodoso la uchunguzi kuhusu ndege hao kwenye Manispaa ya Bukoba, ambapo afisa tarafa ABDON KHAWA ameitoa taarifa hiyo ya kitaalam mbele ya mkuu wa mkoa wa Kagera Fabian Masawe alipotembelea kisiwa hicho jana.


Bwana Kahawa amesema kuwa taarifa hiyo inaonesha asilimia 45% ya mapaa ya nyumba za mabati yamepata kutu na kutoboka kutokana na kinyesi cha ndege. Kulingana na taarifa hiyo asilimia 61% ya kuku na 6% ya mbuzi wamekufa kutokana na vinyesi.
Katibu Tarafa Bwana Kahawaakitoa taarifa kwa RC
Dokta Ruuta mganga mkuu wa mkoa wa Kagera
Mh Diwani kata Miembeni Richard Gasper Asilimia ya wakaazi wa Musira wanaupele na kuwashwa ngozi baada ya uvamizi wa ndege.
Mkuu wa mkoa na wataalamu pamoja na wanahabari wakishuka kwenye mtumbwi
Wakaazi wa Musira wakisikiliza ripoti ya wataalamu wa uchunguzi
Ni Wakaazi wanaugulia ngozi kutokana na kupata upele na ngozi kuwasha.
Hili ni kanisa la Orthodox kisiwani humo, ambalo limezungukwa na miti iliyojaa ndege hao Taarifa rasmi inasema 28% ya wakaazi wamekuwa na tatizo la kuumwa tumbo na kuharisha baada ya uvamizi wa ndege hawa.

Pia wakazi hawa asilimia 43% hawachemshi maji ya kunywa na 4% tu ya wakaazi wa Musira ndiyo wenye vyoo bora.

Hatahivyo sampuli zilizokusanywa na wataalamu kuanzia 11 mach adi 16 mach 2014, yamepelekwa kwa mkemia mkuu, ili kuchunguzwa kutokana na vitedea kazi hafifu katika kituo kilichopo mkoani Kagera, hivyo taarifa zimesubiriwa.
KUTOKA JAMII FORUMS