Adverts

Feb 23, 2011

JAPAN YAAHIDI KUHAKIKISHA KUWA UJENZI WA BARABARA KATI YA MWENGE NA TEGETA UNAANZA MAPEMA MWEZI APRILI MWAKA HUU.

Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Hiroshi Nakagawa (kulia) akimpatia taarifa Waziri wa Ujenzi Mhe. Dr. John Magufuli (Mb) kuhusu maendeleo ya miradi mbali mbali inayotekelezwa chini ya ufadhili wanchi ya Japan.

NA MWANDISHI WETU

    Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Hiroshi Nakagawa amemtaarifu Waziri wa Ujenzi Mhe. Dr. John Magufuli (Mb) kwamba, Serikali ya Japan itahakikisha kuwa ujenzi wa sehemu ya barabara kati ya eneo la Mwenge na Tegeta katika barabara inayounganisha mji wa Dar es Salaam na Bagamoyo, inaanza kujengwa mapema ifikapo mwezi Aprili mwaka huu na kukamilika katika ndani ya muda na kwa viwango vilivyoanishwa katika mkataba.

    Kampuni ya Ujenzi ya Konoike kutoka Japan mnamo mwezi Desemba mwaka jana iliingia mkataba wa upanuzi wa barabara kuanzia sehemu ya Mwenge hadi Tegeta yenye urefu wa kilometa 12.9. Ujenzi huo unagharimu kiasi cha fedha za Kijapani Yen 4.55milioni ujenzi wake unakadiriwa kuchukua miezi 29.

Kukamilika kwa mradi huu kutasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza msongamano wa magari hasa kwa watumia barabara hiii kutoka mikoa ya kaskazini mwa Tanzania pamoja na wakazi wengine wanaoshi katika vitongoji mbali mbali inakopitia barabara hiyo wanaoingia jijini Dar es Salaam. Balozi wa Heshima wa Tanzania kwenye jiji la Osaka nchini Japan ambaye pia ni mmiliki wa Kampuni ya Konoike Dr. Kazusue Konoike (kushoto) akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi Mhe Dr. John Magufuli (Mb), wakati halipomtembelea wizarani hapo kuelezea maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa barabara ya Mwenge hadi Tegeta ambayo ujenzi wake unatarajiwa kuanza mapema Mwezi Aprili mwaka huu
"