Inaonekana hili tatizo la wanaume kupigwa katika ndoa zao ni kubwa. Nimeshangaa kusikia katika video hii kwamba nchini Kenya eti theluthi moja ya wanaume wanakung'utwa majumbani mwao. Pengine ndiyo maana wenzao wa Tanzania waliamua kuanzisha chama chao kabisa. Jamii, hata hivyo, imekazania tu kupigania haki za wanawake. Na wanaume hawa je?