Adverts

Apr 24, 2011

MAKAMPUNI YADAIWA KUTEKELEZA MIKOA YA PEMBEZONI KUDHAMINI

 Makampuni ya simu na yale yanayotangaza bidhaa zake nchini yamelaumiwa kwa kukimbilia kudhamini michezo katika mikoa ya Dar es salaam na taasisi maarufu zinazoandaa mabonanza na kutekeleza maeneo ya vijiji ambako pia vipaji vimeendelea kufukiwa.
Hatua hiyo inatokana na Mabonanza mawili yaliyofanyika miezi miwili mfululizo  katika eneo la Mpakani mwa TANZANIA na ZAMBIA ambapo yaliendelea kuvutia timu nyingi kushiriki ambapo awali zilishiriki timu nne lakini sasa zimefikia timu 10 kutoka mikoa ya NJORUMA na Mbeya ambapo kwa Mkoa wa NJORUMA ulileta timu za Veteran kutoka Njombe na Makambako.
Mkoa wa Mbeya ulihusisha timu kutoka wilaya za Kyela, Mbeya Jiji, Rungwe, Mbeya vijijini, Mbozi na Tunduma  ambayo ni wenyeji walioleta timu nne.
Licha ya baadhi ya makampuni ya simu kufika eneo hilo lakini walionekana kutoonyesha bidhaa zake kutokana na kutojitokeza katika udhamini huo ambao pia libeneke la  http://www.dtwevetz.blogspot.com/ limekuwa  mmoja wa wadau wanaodhamini mashindano hayo kwa kutoa ofa ya matangazo kwenye blog yake na kufuatilia shughuli nzima kila itakapofanyika.
Aidha Blog mama ya http://www.mbeyayetu.blogspot.com/ imekuwa mmoja wa wadau wanaofuatilia kwa karibu mashindano hayo ambayo katika mchezo utakaofuata yatahusisha pia timu kutoka nchi jirani ya ZAMBIA hatua ambayo pole pole yaanza kupandisha hadhi ya michezo ya timu ya veteran huku  matamasha hayo yakitoa fulsa kwa familia kupata mahala pa kubadilishana mawazo na kujenga upendo, urafiki na udugu.


Wadau wa Bonanza wakishiriki katika nyama choma kama sehemu muhimu ya burudani katika michezo hiyo
 Kutokana na kukosekana kwa udhamini wa uhakika katika mabonanza hayo, wabadilisha noti(wanaobadili fedha za kigeni) kutoka eneo la Tunduma walijitokeza kuandaa mashindano hayo kwa kushirikisha wafanyabisahara walioko katika mji wa Tunduma ambapo hoteli ya SASCEE HIGH CLASS, BROTHER K, KIDEVU, na diwani wa mji wa TUNDUMA kuunganisha nguvu za vijana katika kufanikisha mashindano hayo.
Kwa ujumla Bonanza hilo limeonekana kuongezeka mvuto kutoka tukio la kwanza ambapo tmu chache zilishiriki lakni sasa burudani imeendelea kupanda hadhi. Kulingana na taarifa zilizopatikana baada ya michezo hiyo ilielezwa kuwa maandalizi yanafanyika kufanya tamasha lingine katika mji wa Mbalizi mwezi May 20 mwaka huu na baadaye Makambako.
Hata hivyo wadau kutoka Tunduma wamesema wataendelea kuandaa matamasha mengine katika siku za usoni ambapo pia mashindano ya nyama choma, uchomaji wa samaki na upikaji wa chipsi yataaambatanishwa katika kushindanisha vijana ili kujua ubunifu wao katika shughuli hizo.

Mh Diwani wa Tunduma Frank Mwakajoka akisalimiana na wadau wa michezo waliofika uwanjani hapo kufuatilia michezo ya bonanza hilo