Adverts

Oct 7, 2012

CHUO CHA MIPANGO SASA KUJIELEKEZA KWENYE MIGOGORO SERIKALI ZA MITAA


Na Danny Tweve
Dodoma 
MAHUSIANO MABAYA BAINA YA MADIWANI NA WATENDAJI KATIKA HALMASHAURI NYINGI ZA WILAYA NCHINI NI SEHEMU YA MATOKEO YA MFUMO WA UGATUAJI MADARAKA AMBAPO UMEFANYIKA PASIPO KUBAINI MAPENGO YA UELEWA KATIKA MAKUNDI HAYO MAWILI IMEBAINISHWA.

HAYO NI SEHEMU YA MATOKEO YA  UTAFITI  WA MAHITAJI YA MAFUNZO ULIOFANYWA NA CHUO CHA MIPANGO DODOMA KWA  HALMASHAURI ZA WILAYA NCHINI, NA KWAMBA KUTOKANA NA CHANGAMOTO HIYO, CHUO KIMEANDAA MTAALA UNAOLENGA KUJENGA UWEZO KWA VIONGOZI WA VIJIJI, KATA NA HATIMAYE  WILAYANI  ILI KUWEZESHA UTENDAJI USIO NA MIGOGORO

WAKIZUNGUMZA KWA NYAKATI TOFAUTI MAKAMU MKUU WA CHUO HICHO SEHEMU YA RASLIMALI WATU NA UTAWALA BW. TIBELIO MDENDEMI NA MKUU WA CHUO HICHO BWANA CONSTANTINO LIFURILO , WAMESEMA SAMBAMBA NA MAFUNZO HAYO, PIA CHUO KINAENDELEA NA UANDAAJI WA TAARIFA ZA USURI WA HALI ZA KIJAMII NA KIUCHUMI ZA WILAYA ZA MKOA WA MOROGORO BAADA YA KUKAMILISHA WILAYA ZOTE ZA MKOA WA DODOMA

CHINI YA MPANGO HUO, HALMASHAURI ZA WILAYA NCHINI KAMA ENEO MUHIMU LA UGATUAJI WA MADARAKA KATIKA  SERIKALI ZA MITAA LIMEWEKEWA MKAZO KATIKA MAFUNZO  HAYO YATAKAYOHUSISHA VIONGOZI WA  KUCHAGULIWA NA WATENDAJI WAAJIRIWA WA HALMASHAUR AMBAPO  WILAYA YA MBULU KATIKA MKOA WA MANYARA   IMETENGWA KAMA ENEO LA MAJARIBIO  NA MPANGO HUO UTATEKELEZWA KWA USHIRIKIANO  BAINA YA CHUO CHA MIPANGO DODOMA NA NA  SERIKALI YA UHOLANZI

DANNY TWEVE DODOMA

SHERIA YA UKIMWI YA MWAKA 2008 YADAIWA KUWA BUTU INAJIKANGANYA

Washiriki wa mafunzo ya sheria namba 8 ya mwaka 2008 ya kuzuia na kupambana na UKIMWI ambayo ni sehemu ya Kampeni ya asasi isiyo ya kiserikali wilayani Mbozi ya MSCHCD ambapo imebainika kuwa sheria hiyo imekuwa butu baada ya kutekelezwa kwa miaka minne sasa bila kunasa hata mtuhumiwa mmoja licha ya kuwepo kwa kasi ya watu wanaoambukiza kwa makusudi katika jamii

washiriki wakiandika jambo wakati wa majadiliano
Na Danny Tweve
Mbozi

Imebainishwa kuwa tangu rais asaini sheria  namba 8 ya kuzuia na kudhibiti maambukizi ya UKIMWI ya mwaka 2008, wilaya ya Mbozi haijaweza kumshitaki ama kumfikisha mtu mahakamani kwa makosa yanayotokana na sheria hiyo licha ya kuripotiwa mara kwa mara kwa vitendo vinavyoambatana na makosa ya sheria hiyo.

Kaimu Mratibu wa Kudhibiti UKIMWI katika halmashauri ya wilaya ya Mbozi SADNESS NGETWA amekiri kutofikishwa mahakamani kwa shtaka lolote linalohusiana na sheria hiyo , licha ya kuwepo malalamiko kwenye jamii ya vitendo vinavyoonyesha uvunjifu wa sheria hiyo

Wakizungumza kwenye mafunzo ya Utekelezaji wa sheria hiyo wilayani Mbozi baadhi ya wadau kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali na viongozi wa dini na makundi ya watu wanaoishi na VVU wamesema hali hiyo inachangiwa na mkanganyiko wa sheria yenyewe juu ya wakati upi mtu atahesabika anaambukiza kwa makusudi ikiwa sheria yenyewe inazuia taarifa za mtu mwenye VVU kutangazwa.

Mratibu wa asasi ya Maendeleo ya jamii katika Mapambano dhidi ya UKIMWI wilayani Mbozi MSCHCD BI ZAINABU MAJUBWA amesema pamoja na udhaifu wa sheria hiyo, bado kuna umuhimu mkubwa kwa TACAIDS na wadau wa mapambano dhidi ya UKIMWI kuendelea kuisambaza sheria  hiyo ili ijulikane kwa wananchi ambao ndiyo walengwa wa sheria hiyo.
Wadau hao wamesema licha ya kuwepo kwa vitendo vya uambukizaji wa makusudi vinavyofanywa na baadhi ya watu wanaojitambua kuwa na maambukizi, bado kumekuwa na ugumu wa kuwashtaki wahusika kwakuwa taarifa zao bado ni siri na kwamba sheria hiyo imekuwa mwiba kwa wanandoa hasa wakati mjamzito anapoenda kliniki na kubainika kuwa  na maambukizi ambapo imekuwa vigumu kumshirikisha mwanandoa mwenzake kwa kuhofia kuvunja ndoa.

Bwana Loyd Nzowa mmoja wa washiriki katika mafunzo hayo amesema, bado licha ya kuonyesha kupinga unyanyapaa, sheria hiyo haijaweka misingi itakayowezesha utekelezaji wake kuwa usiyo na vikwazo kwakuwa hata upatikanaji wa huduma za tiba bado unachangamoto nyingi hii inatokana na shughuli za UKIMWI kwa ujumla kutegemea misaada kutoka nje  kwa asilimia 90 kitu ambacho hakitoi uhakika wa huduma kwa  WAVIU.

Mafunzo hayo yanaendeshwa na asasi ya Mbozi Society  katika kata tano  ikilenga kueneza sheria  ya Kuzuia na kupambana na UKIMIWI ya mwaka 2008, kwa kujielekeza kwenye vifungu vya 7 na 8 vinavyohusiana na haki  na wajibu kwa  watu wanaoishi na VVU  na nisehemu ya ufadhiri wa Foundation for Civil Society.

Sep 10, 2012

NO maandamano Mikoani! Polisi watahadharisha


Maandamano yaliyopangwa na wanahabari nchini kote kufanyika kesho asubuhi huenda yasifanikiwe kwa mikoani baada ya taarifa za ndani kuonyesha kupenyezwa taarifa kutoka ngazi za juu za jeshi la polisi   zikitaka makamanda kuhakikisha hayafanyiki.
Taarifa kutoka mikoa mbalimbali zinaonyesha kuwa maandamano hayo yamekosa vibali kutoka polisi ambapo mikoa ya Mbeya na  Dodoma hadi saa nne usiku kulikuwa na taarifa za kusitishwa kwa maandamano hayo.
Mkoani  Mbeya wandishi wa habari walikutana kwenye ofisi yao leo jioni ambapo katika hali ya kushangaza watu wanaojiita wadau wa sekta ya habari walifika kuungana na wandishi kupanga namna ya kuandamana ambapo miongoni mwake walishtukiwa kuwa ni askari wa idara ya upelelezi ya jeshi la polisi.
Kutokana na hali hiyo wandishi waliwataka wadau hao wasubiri mazungumzo ya wanahabari yamalizike ndipo waruhusiwe, lakini baadaye wanahabari walikubaliana kutoshirikisha watu wengine kwenye maandamano hayo kwani yanahusu wana taaluma wa habari tu.
Hatua hiyo pia imelenga kuepusha mwendelezo wa ajenda mpya zinazozaliwa kutokana na tukio la kifo cha mwandishi wa habari Daud Mwangosi ambapo wanasiasa na makundi mengine ya jamii yanaweza kutumia fulsa hiyo kupenyeza ajenda zao.
Habari kutoka Dodoma zimesema, wandishi wa habari wa Mkoani humo walipanga kutekeleza maandamano ya amani ya kimya kimya lakini polisi imetoa taarifa kuwa haitaruhusu maandamano hayo kwani hayana kibali kutokana na kuchelewa kuombwa kibali hicho ndani ya saa 12.
Vivyo hivyo Mbeya ambao pia waliomba kibali kwa kuchelewa nao wamepewa taarifa za kuzuiwa maandamano hayo kwa siku ya kesho na kutakiwa kujiandaa kwa keshokutwa jambo ambalo litaenda kinyume na tangazo la muungano wa vyama vya wanahabari na vyombo vingine vilivyotangaza kuandamana kesho.

Aug 14, 2012

PICHA KUTOKA BUNGENI JIONI YA LEO

Waziri wa habari, vijana, utamaduni na michezo Dkt. Fenela Mkangara(kulia) akijadili jambo na Naibu waziri wa Ujenzi Eng. Gerson (katikati) wabunge wa viti maalum Maulida Komu (kushoto) nje ya ukumbi wa bunge ambako mkutano wa nane unaendelea.

Mbunge wa Ilala Mussa Zungu Azzan (kulia) akiongea jambo na Mbunge wa Kigoma Kaskanzini Zitto Kabwe (kushoto) katika viwanja vya Bunge leo mjini Dodoma wakati wakiingia ndani ya ukumbi wa bunge kwa ajili yakuhudhuria mkutano wa nane, kikao cha arobaini na saba kinachoendelea mjini humo.

Msemaji Mkuu kambi ya upinzani wizara ya Maliasili na Utalii Mchingaji Peter Msingwa akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu uamuzi wa Serikali wa kuwafukuza kazi watumishi watatu wa wizara hiyo badala ya kuwachukulia hatua wwatumishi wote waliohusika kwenye sakata la usafirishaji wa wanyama pori kupitia Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro kwenda Quatar. Kulia ni Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi akifuatiwa na Mbunge wa Musoma mjini Vicent Nyerere.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akitoa wosia kwa wanafunzi 20 waliofanya vizuri katika mitihani ya kidato cha sita kwa mwaka 2012 bungeni leo mjini Dodoma. Wanafunzi hao 10 wasichana na 10 wavulana wamepewa cheti , kopyuta ya pakato (laptop) na fedha taslimu shilingi laki mbili kwa kila mmoja.

Wanafunzi 20 waliofanya vizuri katika mitihani wa kidato cha sita kwa mwaka 2012 wakiwa katika picha ya pamoja nje ya ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma. Wanafunzi hao 10 wasichana na 10 wavulana wamepewa cheti na Waziri Mkuu, kopyuta ya pakato (laptop) na fedha taslimu shilingi laki mbili kwa kila mmoja.
Picha na Anna Nkinda – Maelezo

WAZIRI MKUU PINDA ATOA CHANGAMOTO KWA WANAFUNZI KUWA NA NIDHAMU ILI WAFAULU

NA MAGRETH KINABO- MAELEZO, DODOMA
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amewataka wanafunzi wote nchini kuwa na nidhamu , kujituma na kufuata maelekezo vizuri ya walimu wao na kuepuka makundi mabaya ili kuweza kupata mafanikio katika masomo yao.
Aidha Waziri Mkuu Pinda amewaasa wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kuhitimu kidato cha sita wa mwaka huu kutumia uhuru vizuri watakaoupata kwenye maisha ya vyuo vya elimu ya juu bila kurudi nyuma katika maendeleo ya masomo yao.
Kauli hiyo ilitolewa leo na Waziri Mkuu, Pinda Bungeni mjini Dodoma kabla ya kuwatunuku vyeti vya kuwapongeza wanafunzi hao 19 kati 20 waliofanya vizuri katika mtihani huo,kutoka shule mbalimbali nchini, ambapo mmoja wao, Jamal Juma yuko nje ya nchi.
Wanafunzi hao ambao wote walipata ufaulu wa daraja la kwanza katika mtihani huo, saba kati yao wanatoka katika shule ya wasichana ya Marian, watatu Mzumbe, wawili Fedha na wengine wawili Kibaha. Waliobakia mmoja mmoja anatoka Kilakala, Ufundi Ifunda, Tabora girls, Tabora boys, Minaki na Mpwapwa.
“Mmefanya vizuri. Mnastahili ! Hongereni Sana. Tunataka ufaulu wenu uwe mzuri zaidi kwa vile sasa ninyi mnakweda kujenga weledi. Mnakuwa wataalamu wa fani Fulani. Tumieni muda wenu kujifunza zaidi kutafuta maarifa zaidi na kuvumbua mambo makubwa zaidi yatakayowasaidia ninyi wenywe na jamii kwa ujumla kujiletea maendeleo,” alisema Waziri Mkuu Pinda.
Aliongeza kuwa ni vizuri utaratibu huo wa kuwatambua wanafunzi bora uwe endelevu na ikiwezekana wapatiwe fursa ya kuendelezwa katika vyuo vikuu vya kipekee nje ya nchi hususan kwenye fani zitakazojenga uwezo kwa taifa.
Waziri Mkuu alisema kati ya shule 10 ,ambazo wanafunzi hao wanatoka, wawili ni kutoka shule za kata, ambao ni Ester Marcel toka shule ya sekondari ya wasichana ya Olele Kilimanjaro na Brighton Lema toka shule ya sekondari ya Kitangiri, Mwanza.
“Napenda niwape pongezi za pekee wanafunzi hawa kwa jihudi kubwa walizozionesha. Kufaulu kwao kunadhihirisha kwamba shule hizi za kata tukiweka bidii kwa kuziwezesha zaidi zitafanya vizuri zaidi kama ilivyo katika shule nyingine,” alisisitiza .
Waziri Mkuu pia aliwataka walimu wote nchini kushirikiana na wazazi na serikali kwa pamoja kufundisha watoto kwa bidii ili waweze kufanya vizuri katika masomo yao kama wanafunzi hao waliotunukiwa vyeti hivyo.
Kwa upande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa alisema wanafunzi hao watazawadiwa pakato (laptop) na sh. 200,000, pia kila shule iliyotoa mwanafunzi bora itazawadiwa sh. milioni moja katika hafla maalum itakayofanyika jioni.
Wanafunzi hao wanatoka katika mchepuo wa PCM ambao ni 16 na mmojammoja toka mchepuo wa PGM, CBA, ECA na HKL.
Naye Spika wa Bunge la Jamhuri, Anna Makinda aliwataka wanafunzi hao kuwa makini na makundi kwa kuyasilikiza huku wakitumia akili zao huku akitoa changamoto shule nyingine kujitahidi kufanya vizuri.
MWISHO.

TAASISI ZA WAMA NA EOTF HAZITUMII RASILIMALI ZA SERIKALI

NA MAGRETH KINABO- DODOMA, MAELEZO
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora,Kapteni George Mkuchika amesema kuwa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo(WAMA) na Taasisi ya Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote(EOTF) zilianzishwa na kuandikishwa kwa mujibu wa sheria inayotawala taasisi hizo na wala hazitumii rasilimali za serikali.
Kauli hiyo ilitolewa na Waziri Mkuchika wakati akijibu swali Bungeni la Mbunge wa Viti Maalum(CHADEMA) , Naomi Kaihula ililoulizwa na Leticia Nyerere Viti Maalum (CHADEMA) kuwa kuwekuwepo na tabia ya wake wa marais hapa nchini kuunda NGO’S na kuzisajili kama taasisi zao binafsi wakati zinatumia rasilimali za serikali.
Je seriklai itaweka lini utaratibu wa kufanya taasisi hizo ziwe za kisheria ili hata wake wa marais wanapomaliza muda wao wapokezane vijiti kana urais unavyofanywa.
Waziri Muchika akifafanua kuhusu swali hilo alisema ni kweli zipo taasisi zinazoendeshwa wake za marais .Hivyo taasisi hizo hufanya shughuli zake kama zilivyo taasisi nyingine zisizo za kiserikali. Ipo taasisi ya WAMA iliyoanzishwa na Mke wa Rais wa Awamu ya Nne Mama Salma Kikwete na EOTF iliyoanzishwa na Mke wa Rais wa Awamu ya Tatu , Mama Anna Mkapa
Aliongeza kuwa kama zilivyo taasisi zingine za hiari na zisizo za kiserikali (NGO,S). Taasisi hizo ziliundwa kutegemea na jinsi Mke wa Rais navyopenda kujishughulisha na shughuli za kijamii.
Alisema inawezekana kabisa akatokea Mke au Mme wa Rais ambaye hana utashi au mapenzi ya kujishughulisha na shughuli za kijamii. Hivyo kutokana na mazingira hayo serikali haioni sababu za kuweka utaratibu wa kufanya taasisi hizo ziwe za kisheria ili wake / waume za marais wanapomaliza muda wao wapokezane vijiti.
Aliongeza kuwa kwa kufanya hivyo tutakuwa tunawalazimisha kufanya shughuli wasizo na utashi nazo.
Akijibu swali la nyongeza la Leticia liliouliza kuwa Watanzania wananufaikaje na taasisi hizo bila tofauti za kiitikadi. Waziri Mkuchika alisema hakuna anayefanya kazi kwa kubagua na alizipongeza taasisi hizo kwa kufanya kazi mijini na vijijini huku akiwataka Watanzania kuanzisha taasisi mijini na vijijini .
Alisema jumla ya wanafunzi 939 wamenufaika kielimu kupitia (WAMA). Pia WAMA imetoa msaada wa vitanda na magodoro katika wodi za wakina mama na imetoa kiasi cha fedha sh. milioni mbili kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wanawake ya MEWATA, ambazo ni msaada kutoka Taasisi ya Nakayama, Japan.
Aidha alisema ina mpango wa kutoa vifaa vya hospitali vyenye thamani y a dola za Marekani milioni tatu kupitia msaada wa Project Care, Marekani vinavyotarajia kuingia nchini.
Alisema taasisi ya EOTF imetoa mafunzo kwa wajasiliamali mbalimbali.
Mwisho.

Aug 11, 2012

HATIMAYE NYENYEMBE AREJEA KUVAA VIATU VYAKE KLABU YA WAANDISHI WA HABARI MBEYA

Mwenyekiti mpya wa Mbeya Press Club aliye simama ndugu Christopher Nyanyembe akitoa Shukrani zake
Ilikuwa ni mapema baada ya uchaguzi ambapo kiongozi mpya Christopher Nyanyembe alipongezana na mpinzani wake, kiongozi huyo mpya ameshinda kwa kura 27

 Waandishi wa habari wakiwapongeza viongozi wapya
Hii Ndio kamati kuu Iliyo chaguliwa katika kuendesha Klabu ya waandishi Mbeya, akiwemo mwandishi mkuu wa Mbeya yetu Ndugu Joseph Mwaisango wa Kwanza kulia kwa walio simama.

KUTOKA MBEYA YETU BLOG

Aug 10, 2012

MKUTANO MKUU WA MBEYA PRESS CLUB WAENDELEA KYELA

Mwenyekiti wa Mbeya press club Christopher Nyenyembe akizungumza kwenye mkutano mkuu ulioketi wilayani Kyela ambapo wadau wa sekta ya habari wameshiriki kupima na kutathmini maendeleo ya sekta hiyo mkoani mbeya
Mwenykiti wa Halmashauri ya wilaya yaKyela akifungua mkutano huo

Beyonce and Jay Z Named World's Highest-Paid Celebrity Couples

Forbes Magazine just named Jay and Bey the highest paid celebrity couple in the world. Together they made $78 million - from May 2011 to May 2012. Beyonce - $40m, Jay Z - $38m. And Beyonce took a break for most of the year. Na wa o! :-)



 From Forbes Magazine,

Take Beyonce Knowles and Jay-Z, for example. Last year’s runners-up on the list of The World’s Highest-Paid Celebrity Couples, the duo has now climbed one spot to top this year’s ranking. Knowles, who took a break from her hectic touring schedule in 2011 to give birth to daughter Blue Ivy Carter, still collects big paychecks from old hits. Besides, the singer’s new album went platinum in the U.S., not to mention her non-musical ventures and endorsement deals, which all helped to bring her total earnings between May 1, 2011 and May 1, 2012 to $40 million, according to data from the latest Celebrity 100 list.
And as the male half of music’s first couple, Jay-Z isn’t far behind his wife. The hip-hop mogul made millions from Watch the Throne, his musical collaboration with pal Kanye West, and even more from the tour that followed. Add to that a bevy of non-musical enterprises such as ad firm Translation and cosmetics company Carol’s Daughter and the result is a staggering $38 million that he has brought home in twelve months, putting the couple’s annual income at $78 million.

Dear lord, what happened to Naomi Campbell's hair?

 
This is a clear example of what happens when we women keep wearing weaves over an extended period of time. But some of us can't just do without our weaves..